NINAPOBANWA.
Kupapatika kwa mtima wangu kunazua maswali ainati yanayohitaji ufahamu angavu katika ulingo wa siasa. Mashaka ya wzpiga kura takriban milioni ishirini na mbili nchini yamejaa moyoni. Nimeamua kufanya fundo siku ya mashaka, fundo yangu ni kupitia uandishi uliosheheni maswali kwa wanasiasa tuliowatuma kwa tasihili lakini wametughafali na kutupuuza. Wengi wenu mmetulekeza wenzenu tuliodamka alfajiri kuenda kituoni kuwaajiri, huku umande na baridi shadidi zikishirikiana kutuadhibu. Mara ngapi tunawaamini hasa mnapokuwa wastaraabu kutuomba kilicho chetu tukijua mtatuauni lakini hatimaye yanapotimia hamtujali tena . Kila mkija hoja na maoni yetu mnapokea kwa ufasaha na usanifu wa kumithilika tusijue kuwa mnatupatia tu usikivu lakini asilani moyo usielewe. Vipi kuhusu zahanati zile tuliowaambia kuwa zina uchache wa dawa? Ni mabadiliko yepi mpaka hospitali kuu ya kaunti in vitanda vya teremka tukaze?
Sisemi kitu labda mwataka tufe halafu matabibu nao watufuate kisa kikiwa ni njaa inayowakabili na kuwakingama kuhudumia wagonjwa kwa utuvu unaohitajika. Mnatuzika katika kaburi la sahau maadamu tulikosa busara tukakubali vibaba vyenu vya unga na shilingi Mia zenu na sasa twaathirika si haba laiti tungeenga kabla kujenga.Si kuzoroteka kwa uchumi, si bei za bidhaa za kimsingi kupanda maradufu na hamjali hambali wala wengi hawana maono ya kutukwamua kiuchumi. Azimio lenu ni kurudi kutufumba macho tena, Aise! Tumekengeuka kupevuka kimawazo,tukikuita jagina basi nenda ukatupiganie.Tusioneane mashaka urafiki wetu ukaisha.
Ni kweli tungeenga kabla kujenga
ReplyDelete👏👏👏
ReplyDeleteinakera sna
ReplyDeleteVizurii sanaa
ReplyDeleteKazi nzr
ReplyDeleteKazi nzuri
ReplyDeleteNice
ReplyDeleteSadakta mkuu ,,ufanisi Ni Waki,,,ueledi unao,,,endelea vivyo hivyo
ReplyDeleteKazi safii kabisaa
ReplyDeleteUzuba tuliokuwa nao hapo awali umetutoka njama zao tumezijua hawatudanganyi tena
ReplyDeleteWueeeh this is nice
ReplyDeleteTungo lenye busara
ReplyDeleteTumechoka!
ReplyDeleteLazima tufunguke macho
ReplyDeleteKazi nzuri
ReplyDeleteNice
ReplyDeleteKazi nzuri
ReplyDeleteKuntu !
ReplyDeletePongezi 👏👏
ReplyDeleteKazi nzuri
ReplyDeleteNakubali
ReplyDeleteHeko!
ReplyDelete